Monday, August 5, 2013

Zivunje....

Leo nataka tuongelee laana za kurithi..wengi tukifikia hapa tunajisahau kabisa haswa kwenye mambo ya ndoa na uzazi, wakati unataka kuolewa je unakuwa umevunja laana za ulipotoka?? na ulipo je umevunja laana za wazazi na mababu ambazo zimekuwa kwenye damu yako??? unajikuta mtu umepata mume unaolewa halafu mama yako hajawahi kuolewa na babu yako alioa wake watano wewe inakuweka wapi sawa unajihisi mwenyewe unabahati lakini je kwanini watu wako nyuma hawakufurahia maisha ya ndoa????au wewe mama yako alikuwa na baba yako akaachika akapata mwanaume mwengine akaolewa na kwa huyo baba alikuwa mke wa pili na wewe mtoto wake umepata mume unataka kuolewa umevunja laana???? au unaolewa na mwanaume ambaye amelelewa na mama tu kwakuwa wazazi wake waliachana kwa sababu ya umalaya, au uchawi je umevunja laana?????... ndoa nyingi zinakuwa hazidumu sio tu kwa umalaya pia laana sasa kwenu nyie hamna hulka ya kudumu kwenye ndoa, mama yako ndoa hana, kaka zako wameachika, dada zako hawana ndoa wewe utaipataje na kudumu kwenye ndoa???? mama yako alikuzaa wewe tu, mama yako mkubwa hajawahi kuzaa mjomba wako anawatoto wawili tu wewe unaingia kwenye kwenye ndoa una mwaka wa tatu hujazaa umevunja laana?? kwenu hakuna hata mtu aliyedumu kwenye ndoa leo wewe umeolewa umezaa watoto je umewavunjia laana katika maisha yao maana MUNGU alisema nitakulaani wewe na uzazi wako wote!!!jamani tunavunja laana..mama yako alipata mimba akifanya umalaya humjui baba yako umalaya ukakusomesha mpaka hapo ulipofikia na wewe unatafuta mume je umevunja laana??? matatizo mengi sana tuliyonayo katika maisha yetu ni kwa sababu ya laana tulizo ridhi kutoka wa mababu na wazazi wetu tujifunze kuvunja laana ili tusihi kwa raha na kuweza kudumu katika ndoa pia tuheshimike kwa jamii...