Monday, August 5, 2013

Itakusaidia...

MWANAMKE katika mahusiano yako usiogope mpenzi/mume wako kuwa na hawara, wala usitumie muda wako kuanza kumchambua mwanamme,kumfwatafwata na kutaka kujifanya kama wewe ndio mama yake umcontrol maisha yake wanaume hawapendi mwanamke wa aina hii..kaa tulia tunza penzi lenu, jiheshimu,mpende beba mapungufu yake kama msalaba wako, mpendezeshe, jifunze kumridhisha kila idara kwa kiasi...mfanye mwanaume wako ajuwe hawezi kuishi bila wewe, awe anakuhitaji kama hajakuoa akuoe na kama amekuoa ashindwe kukuacha..hapo ndipo atakusifu na watu wote watajuwa wewe ni mke uliyetoka kwa MUNGU...kila mara jitahidi kumpenda kama hujawahi kupenda tena yani awe na furaha akiwa na wewe na kutaka kila mtu ajuwe umuhimu wako kwake....hayo mambo ya hawara na kufumaniana ni ya mpito tu mwisho wa siku ni wewe na yeye na mapenzi yenu umeweza kutunza kiapo ulichoweka siku ya ndoa, umeweza kumtunza mume na watu wakaona kweli ametunzika, watoto wenu mnawalea kwa maadili ya MUNGU, wewe mwenyewe unajiheshimu kama mke wa fulani????????....TAFAKARI