Tuesday, August 6, 2013

Word...

Baadhi ya wasichana wanapoona maisha ni magumu, kila analojitahidi kufanya halifanikiwi, hakuna pa kukimbilia wala msaada wanaona lililobaki ni kuolewa. Wanafikiri kuolewa kutawaondolea matatizo waliyonayo, watapata mahali pa kuishi, mtu wa kumtunza, atafanya analotaka na kila alilokuwa analitamani atalipata. Wanaingia kwenye ndoa kukimbia matatizo waliyonayo, wanaingia kwenye ndoa wakimuona mume kama mzazi wa kumtunza. Wanapokuta hali sio kama walivyotarajia ndoa inaishia kuwa ndoano na msalaba usiobebeka.
Usione maisha ya ndoa ya fulani ukayapenda ukajua nawe itakuwa hivyo. Usitumie mfano wa fulani nawe kufanya jambo. Hujui mtu huyo amepitia na anapitia nini. Mungu pekee ndiye kimbilio na msaada, zaburi 46:1-2. Usifanye uamuzi mkubwa kama kuolewa sababu ya matatizo yanayokuzunguka, hiyo sio sababu kabisa ya kuingia kwenye ndoa. Matatizo yapo kwa wenye ndoa na wasio na ndoa na msaada wa wote ni Mungu. Jifunze kumtegemea Mungu 100% kabla hujaingia kwenye ndoa.

Source: Women of Christ