Tuesday, August 27, 2013

Word..

Hii imewatokea wengi. Familia za kiafrika jambo la kukaa na ndugu ni la kawaida kabisa na wengi wetu kabla hatujaishi wenyewe tumeishi kwa ndugu. Sasa kuna jambo huwa linasumbua watu wengi, unakuta unaishi na mtu vizuri, unakaa naye kama mwanao means unamjali, unamtimizia mahitaji yote na vile vile akikosea unamkanya. Lakini unakuta mtu huyo hawi na furaha wala kuchangamka akiwa nawe, ila akiwa na watu wengine yupo more than happy. Anaweza kuwa mdogo wako, dada/ kaka yako, wifi, mkwe, mpwa, n.k.
Hali hii husababishwa na nini? Je ni kiburi au nidhamu ya woga? Na mtu wa aina hii unaishi naye vipi?

Source:Woman of Christ

0 comments:

Post a Comment