Friday, August 23, 2013

Word

Wasichana wengi wa siku hizi wanapenda sana maisha super. Wanataka wampate kijana aliyejikamilisha au angalau awe na degree na gari. Utakuta msichana yupo kwenye mahusiano na mkaka na amekubali kuoana naye, baada ya muda kupita anakuja kijana msomi mwenye hela na gari anamtosa mchumba wake na haraka unasikia harusi. Wakaka wengi sana wamejeruhiwa kwa sababu ya kuachwa na wachumba zao kuolewa na wenye hela zaidi yao.
Hivi unawezaje kumuangalia mtu leo ukajua hatima ya maisha yake? Kama ulikuwa humpendi ni kwanini ulikubali ombi lake na ukawa naye na akakutambulisha kwa marafiki na baadhi ya ndugu? Kama unaona hujampenda mkaka na wala Mungu hajasema nawe kuwa ndiye, kwanini umkubalie? kumbe wewe unawapanga uone nani mambo safi zaidi ndio uolewe naye? Acha tabia hiyo maana hata ukiingia kwenye ndoa na mumeo akatetereka kiuchumi utakuwa rahisi sana kumsaliti kwa wenye mali.
Kama unatafuta kuolewa ili upate wa kukuvisha na kukupatia fedha please kuna better alternative ambayo ni kutafuta kazi na kuifanya kwa bidii. Ndoa sio gari, nyumba, fenicha, wala fedha.

Source:Woman of Christ

0 comments:

Post a Comment