Wednesday, August 21, 2013

Ubinafsi...

Katika mahusiano haswa kwa wale ambao ni wachumba wanaoelekea kwenye ndoa ama kwa wale walio kwenye ndoa hakuna kitu kibaya kama ubinafsi, ubinafsi haurekebiki wala hauna tiba heri upewe umbea kuliko ubinafsi na ni mbaya ukipewa vyote viwili..mahusiano mengi hayadumu kwasababu ya ubinafsi mnapoamua kuwa pamoja kila kitu ni chenu wote sio chako wala chake matatizo yanaingia pale mnapogombana na hii sana ni kwa walio ndani ya ndoa utakuta tena mmegombana na mwenzako basi kama ulikuwa unataka kumfanyia jambo zuri humfanyii tena, labda ulitaka kumnunulia gari mkeo kisa mmegombana kakununia siku mbili tatu unagairi tena humnunulii au mke unataka kumnunulia mumeo suti mpya kisa amerudi usiku wa manane unagombana hata hutaki tena kumfanyia jema wala kumnunulia tena ulichotaka kumpa..hii ni mbaya sana na nikukomoana tukiishi maisha ya kukomoana na ubinafsi kisa ni chako hutaki kumpa mwenzako hatutafika..MUNGU alimuumba mwanaume kuwa kichwa cha familia mwanamke acha ubinafsi muweke mumeo mbele awe kichwa hata kama umempita kipato sio kila mtu ajuwe wewe ndio unaendesha familia muache baba awe baba, na unapoingia katika ndoa kwa mguu mmoja nje na mwengine ndani lazima utakuwa mbinafsi utaogopa kushirikiana na mwenzako ukijuwa kesho tukiachana je kitu changu hiki nitakipataje..jamani hayo sio maisha  lazima kila kitu unachotaka kufanya maishani ukifanye on your best ingia kwenye ndoa kwa miguu miwili hata kama wewe ndio unakipato kuliko mumeo mnapokuwa sehemu ya wazi muache mumeo awe mumeo mpe heshima yake kama wewe ndio unatakiwa kulipia kitu fulani mbele za watu kabla hamjashuka kwenye gari au kufika hiyo sehemu mpe mumeo hela alipe yeye mkifika inampa security na kujiona yeye ni mwanaume..na sio mkigombana unamnyali kwa watu mwanaume mwenyewe miye ndio nakuweka ndani nakuhudumia na kukupa kila kitu..leo MUNGU amekubariki mwanamke/mwanaume unavyo hivyo ulivyokuwa nazo anauwezo wa kugeuza shilingi upande wa pili akipewa mwenzako itakuwaje??? ataishije na wewe?? TAFAKARI

0 comments:

Post a Comment