Wednesday, August 21, 2013

Word

Furaha haitafutwi kwa jirani. Moyo wa kuchangamka hautokani na mali. Amani haitokani na kukosa matatizo. Unapaswa kuwa na moyo wa shukrani (heart of gratitude) ili uweze kuwa na furaha, amani na moyo uliochangamka. Unaowaona wana furaha na moyo uliochangamka sio kwamba hawana matatizo au wanawatu wa kuwachangamsha la bali wana moyo wa shukrani kwa Mungu wao kwa kila kitu. Kila wakati wanayaona yanayowapasa kumshukuru na sio kuangalia wasivyonavyo.
Mtu mwenye moyo wa shukrani lazima atakuwa mwenye furaha, amezungukwa na marafiki, ana amani, mjasiri na anayejiamini, muwazi na rahisi kuwasiliana naye. Mtu asiye na moyo wa shukrani mara zote yupo mwenyewe, anahasirahasira, hana furaha, hajiamini, anaona kila aliyefanikiwa zaidi yake analazimika kumsaidia, sio muwazi.
Hata maombi pia yanaonyesha maana mwenye moyo wa shukrani maombi yake yamejaa sifa na shukrani kwa Mungu na yule asiye na shukrani maombi yake yamejaa laumu na manung'uniko.

Source: Woman of Christ

0 comments:

Post a Comment