Tuesday, August 20, 2013

I WANT TO SAVE A LIFE...DO YOU??

Wapendwa MUNGU ni mwema na anatupenda sana, sisi tuliobarikiwa kuwa salama leo, wenye afya na tunahema na kufurahia maisha, lakini tukumbuke kuna wenzetu wanaumwa wapo mahospitalini bila msaada zaidi tu ya kumtegemea MUNGU, nimeguswa sana tokea asubuhi nikaongea narafiki yangu wa karibu ya kwamba ninawito ndani yangu ya kutoa damu ambayo itasaidia watu wanaokuja hospital wakihitaji damu, wagonjwa wengi katika mwaka wanahitaji damu, labda umeshaona ndugu yako, rafiki yako, jirani yako,mzazi wako,mume/mke wako au hata mtoto wako anahitaji damu na ukaweza msaidia ila kuna wale ambao wanahitaji misaada na wanategemea tu sisi ambao tunauwezo wa kutoa damu ndipo wapewe wao nakumbuka babu yangu kabla hajafariki mwezi wa tano aliumwa sana siku tumempeleka hospital alitapika karibia beseni zima la damu, tukiwa tumekaa reception muhimbili madaktari wakaamuru awekewe kwanza drip ya damu kabla hajapelekwa kulazwa maana asingeweza kufika chumbani kama angekuwa hajaongezewa damu nashukuru kwa damu zilizokuwepo siku hiyo mpaka akapewa japo siku tatu baadaye alifariki, ndio maana nikawaza i want to save a life japo kwa siku tatu tu huyu baba aweze kumwambia mkewe jinsi anavyompenda, huyu mama aweze kuwabariki watoto wake kabla hajafa..siku tatu ni masaa mengi sana ya kubadilisha mtu na dunia..ndio maana 21/9/2013 ni siku ambayo mimi, wewe na yule tutakayoenda damu salama kwenda kutoa damu ili ziwasaidie watu hata kwa siku tatu tu, tuendelee kula matembele kwa wingi na virutubisho vya kujaza damu zetu..tafadhali kama na wewe ni mmoja wa watu unaotaka kushiriki naomba unipetaarifa mapema nikuweke katika maandalizi ya siku hii 0717 019320...MUNGU awabariki sana

0 comments:

Post a Comment