Monday, August 19, 2013

Kuelekea kupata mtoto...

Nataka niongee na wanawake ambao hawajazaa na wanawake ambao wanamimba, unajuwa wewe kama mwanamke ni mtu wa thamani sana duniani bila wewe dunia itakuwa tupu, ni wewe unaweza ukazaa watoto wenye baraka na ni wewe unaweza ukazaa watoto wenye laana kabla hujapata mimba pindi unapoanza kumjuwa mwanaume hakikisha mara kwa mara unaombea tumbo na uzao wako utafanyaje huwa napenda kuwashauri wanawake vyumbani mwao wasikose mafuta ya nazi ama ya olive oil utayaombea hayo mafuta kwa dini uliyonayo mimi huyaombea na kuyageuza kuwa damu ya yesu, basi kila utakapokuwa unaombea tumbo lako utajipaka na kuanza kuongea na MUNGU kuhusu uzao wako kama hujazaa utaomba MUNGU akubariki tumbo lako likapate kubeba mimba kwamba hatakama kuna wagumba kwenye ukoo wenu lakini wewe utazaa kataa hali na roho ya ugumba na ukazae tu na mume wako au na mwanaume MUNGU aliyekupangia kataa kuzaa na mume wa mtu kwani watoto wengi wa wame wa watu hawathaminiwi wanafichwa hawatambuliki na utakapokuwa umebeba mimba kila siku asubuhi paka tumbo lako na yale mafuta muombe MUNGU akulindie mtoto wako kila siku, mwanao akitoka afanane na baba yake au wewe mama yake, akawe mtoto wa baraka, mvunjie laana zote za ukoo kabla hajatoka, kataa mimba kuharibika, muombee akija duniani akapate kuwa baraka kwa watu na sio laana, muombee akawe na akili kabla hajaanza hata kuongea,usisahau kumuombea kuwa mcha MUNGU maana huo ndio wingi wa maarifa...TUJIFUNZE kuombea matumbo yetu dunia inaharibika na kubarikiwa kwasababu ya tumbo la MWANAMKE...

0 comments:

Post a Comment