Sunday, August 11, 2013

Tumejikongoja kidogo..

 Jumanne nilituma post kuhusu huyu baba anayeomba masaada wa fedha ili aweze kupata ticket na passport kwa ajili ya kwenda India kumtibia mwanae ashura ambaye ana cancer ya ngozi...

Kwa uwezo tuliokuwa nao mimi na marafiki zangu wengine tuliweza kujichangisha kwenye group yetu ya wanawake ya Reserve ikiongozwa na admin wetu shoga yangu kidawa Lamkeku tukaenda zetu mpaka mkuranga huko kupeleka hela kwa kina Ashura.

 Hali ya Ashura kwakweli ni mbaya vidonda vinatoa harufu na kuanza kuoza, ila bado naamini MUNGU yupo upande wake watakamilisha na kumsafirisha huyu mtoto akatibiwe...na wewe kama umeguswa na ugonjwa huu please rejea post yangu ya nyuma ya msaada kuna number ya simu ya baba yake ashura umtumie kidogo ulichokuwa nacho MUNGU atazidi kukubariki...

0 comments:

Post a Comment