Tuesday, August 6, 2013

Mwanamke unapofikiria kuolewa...

Kuna umri ukifika mwanamke unataka kuolewa, uwe na watoto na mji wako lakini kabla hujapata hivi unajitunzaje kama mwanamke anayetaka mume, na unampataje huyo mwanaume wa kukuoa, ama wewe ndio wale wanaokuwa na wanaume watatu au zaidi wakiangalia yupi ataoa unakula huku na huko, au wewe ndio yule mwanamke unayekuwa na mahusiano na mume wa mtu wakati unangojea wako,au ni wewe mwanamke uliyemuachisha mume mwanamke mwenzako ukisubiri kuolewa wewe...wengi wetu ndoa zetu hazitufikii kwa sababu ya majanga kama haya, tunajiachia sana kuchezewa na wanaume mpaka nyota yetu na baraka za kuwa wake zinafifia, wakati unasubiri kuwa mke mwema wa fulani jifunze kumuomba MUNGU akupe mume wa ubavu wako wa kutoka kwake ni sala tu ndio itakupa wewe mume na ndoa yenye matunda mema na kama una mwanaume mmoja muombee mwanaume wako kama kweli ni mumeo akuoe na kama sio badi MUNGU amuweke pembeni asimzibie njia mumeo aliyenjiani kuja kwako..Mwanamke kataa kuchezewa na kuchakazwa na wanaume wewe ni mtu wa thamani sana.