Friday, August 16, 2013

Nimepata maswali mengi kuhusu wanaume kwanini wanaume wengi hawawezi kutulia na mwanamke mmoja ilianza hivi twende kwenye biblia MUNGU alimuumba mwanaume na katika ubavu wake wa kushoto akatoa ubavu mmoja na kumuumba mwanamke na akawaambia wafanye yote kwenye bustani lakini wasile matunda ya mti mmoja ambao walikatazwa, na kweli walifanya hivyo mpaka shetani alipokuja kumpotosha mwanamke na mwanamke naye akampotosha mwanaume wakatenda dhambi na ndipo matatizo yalipoanza hapo duniani na tokea siku hiyo mwanaume akawa mtumwa kwa mdhaifu sana mbele ya mwanamke iwe kwa mazuri ama mabaya mwanamke anauwezo wa kuulainisha moyo wa mwanaume na kumfanya afanye atakayo mwanamke, twende kwenye mahusiano tuongelee wanawake ambao wanatongozwa na mume wa mtu na wanajuwa kabisa ni mume wa mtu lakini bado anamkubali sio kwamba anapenda bali ni shetani anajitumia tena kwa mwanamke kuharibu ndia ya huyo mwanamke na ukiangalia mwanamme anavyomtongoza mwanamke atampa sababu mbaya kibao anazofanya mkewe ili aonewe huruma na kukubaliwa na mengi huwa niuongo lakini wanaume wameshajuwa jinsi ya kulainisha wanawake, na shetani pia atajiingiza kwa mwanamke kujitongozesha kwa mume wa mtu sio kwamba anapenda bali ameshikwa na shetani na yeye mwenyewe hajielewi..lakini kama leo tungesema hatutaki kutumiwa na shetani kuharibu ndoa za watu kweli wanaume wangejirekebisha lakini kwakuwa na sisi tunakubali kutumiwa katika mipango ya shetani kwa kutupa matatizo kibao ambayo tunajuwa tutatatuliwa na wame za watu tunajikuta tunajiingiza katika mpango wake wa kuharibu ndoa..maana shetani ameshajuwa sasa hivi mahali pa kushindana na MUNGU ni kwenye ndoa hapo ndio anapata wafuasi wengi maana watu sio wavumilivu tena, watu wanapenda maisha ya haraka ukikutana na viserengeti boys vinapendeza kwasababu ya mke wa mtu mmama mtu mzima utashangaa na ukikutana na msichana mdogo anamkatikia kiuno mbaba anayeweza kumzaa mara mbili utashangaa..ukimkuta kijana kaoa hana hata mwaka analala nje ya nyumba yake utashangaa ukikutana na mwanamke aliyeolewa anakumbatiwa na kukatiwa kiuno na mwanaume aliyeoa ambaye sio mume wake utashangaa..huu wote ni mpango wa shetani na wengi tumeingia, wameingia na bado wanaendelea kuingia bila kujijuwa...haijaanza jana wala haitaisha kesho MPAKA UTAKAPOJITAMBUA NA KUTAMBUA UMUHIMU WA HIYO NDOA ALIYOKUPA MUNGU NA UTAKAPOJITAMBUA THAMANI YAKO KAMA MSICHANA SIO KUTUMIWA HAPO TU NDIO DUNIA ITABADILIKA ZAIDI YA HAPO bado tupotupo sanaaaaa

0 comments:

Post a Comment