Wednesday, August 14, 2013

Juwa ya kwamba...

Kila mtu anaingia kwenye ndoa kwa malengo ya kwamba ndoa yake idumu milele, wazae watoto na wafurahie kuwalea pamoja, ni furaha ya kila binadamu unapopata ndoa, tunapofika kwenye ndoa pale ndio balaa zinapoanza pindi ambapo mke anataka afanyiwe hivi na mwanaume anataka afanyiwe hivi tunaposhindwa kukutana katikati katika kukubaliana tuishi vipi ndio balaa zinapoanza, wanawake tunapoingia kwenye ndoa tunataka kupendwa, unithamini, utumie muda wako mwingi kuwa na mimi mwanamke anataka kumuhudumia mumewe muda wote wawe kwenye furaha mwanamke anaacha kila alichokuwa nachokibaya zamani akiolewa wanaume wa mwanzo wote wanapigwa chini akili yake ni kwa mumewe tu, mwanaume je yeye anaingia kwenye ndoa kwamba sasa ameshakuwa anataka kuwa namaisha yake awe na nyumba yake na mkewe, afuliwe, apikiwe, mpate watoto aheshimike kuitwa baba lakini je anakuwa ameachia wanawake wake wa nyuma au anakuwa amejipanga kwamba mpaka kufa ni mimi na mke wangu hapana, wanaume wengi ndoa ni step tu nyengine ya maisha sio kwamba ndio wamefungwa wasiwe na wanawake nje japo wanajuwa hairuhusiwi lakini wengi hawawezi..sasa pale mwanamke unapokuja kugundua mumeo ana mwanamke nje ndipo unapoanza kuchanganyikiwa, kukosa amani ya kukaa kwenye ndoa, mapenzi kwa mumeo yanapungua unajikuta huwezi kumuhudumia tena vyema mwanaume unamaumivu wengine mpaka wanakonda na kuumwa hadi kulazwa, wengine wanaona haifai kama kaniona wa nini na mimi nitamuona wakazi gani unaamua kuacha ndoa yako na kuondoka, huku labda ukiwa na mwanao ndoa unaiacha kwa maumivu na majuto laiti ningejuwa asingenioa..kama huyu ndio atakuwa mwanaume wako wa mwisho basi hata mimi nakushauri uondoke lakini kama bado baadae utataka kuwa na mwanaume mpaka utakapokutana na mwanaume ambaye kweli yupo tayari kukaa chini na mwanamke mmoja na kumtumikia basi wanaume wote wapo kama mumeo unayemuacha utamkimbia tena na tena na tena utakimbia mara ngapi?????? hakuna aliyesema ndoa ni rahisi toka enzi za biblia ndoa ni ngumu,majaribu,mapito na kukata tamaa lakini ukimruhusu aliyekupa ndoa aisimamie hata ukipita magumu gani atakuonyesha jinsi ya kutokea maana yeye sindiye aliyemuumba mumeo na mkeo basi anajuwa jinsi gani yakumuweka sawa..TAFAKARI HILI UNAPOFIKIRIA KUOLEWA AU KUOA MAANA KUNAWANAUME PIA AMBAO NDOA ZAO ZINAWAKA MOTO WAKE ZAO HAWAKAMATIKI...

0 comments:

Post a Comment