Wednesday, August 14, 2013

Word...

Nani kakuambia kuwa sababu tu mtu anaimba praise madhabahuni basi hawezi kuwa HIV+?
Nani kasema kuwa sababu tu mtu ameokoka tangu shule ya msingi basi hawezi kuwa hiv+?
Kuhubiri, kuvaa nguo ndefu, kuomba kwa machozi mengi, kuvaa tai, kuokoka hakumuondolei mtu possibility ya kuwa HIV+.

Vijana wengi siku hizi tena wanaosema wameokoka wanashiriki tendo la ndoa kwa kigezo kuwa wamekubaliana kuoana hivyo haina tatizo. Wamezoelea dhambi kiasi kwamba dhamiri zao haziwasuti na wanaendelea na huduma. Hofu ya Mungu imewaondoka kabisa. Muogope Mungu, kimbia dhambi, ishi maisha matakatifu hata kama watu watakucheka na kukuona mshamba. Tafuta kumpendeza Mungu na sio wanadamu.

Source:Woman of Christ

0 comments:

Post a Comment