Monday, August 12, 2013

MWANAMKE: nataka niongee na wanawake ambao wapo kwenye mahusiano ambayo yanaelekea kwenye ndoa na pia wanawake ambao wapo kwenye ndoa jamani aihusu kabisa wewe kumwambia mwanaume wako mambo ya nyumbani kwenu ambayo unaona hayana faida ya yeye kuyajua, yani kunawanawake hawana siri kila kitu cha kuhusu maisha yake wanamwambia mwanaume mengine ni aibu kabisa mwenyewe unasema oohhh namwambia ili akija kusikia asidhani nimemficha jamani hebu chuja ya kumwambia mwanaume kwasababu kama hujui wanaume wanatumia mabaya na mapungufu yako na familia yako kama fimbo ya kukuchapia wewe baadae ndani ya ndoa nitakupa mfano " mpenzi yani hapa ninahasira baba jana karudi saa nane za usiku akaanza kugombana na mama akampiga kweli" atakwambia pole basi utajibembelezesha yataisha sasa amekuoa wewe ikafika siku na yeye akarudi saa nane za usiku mara tena wewe ndio umevimba na kununua kwa hasira unamuuliza na kutaka kugombana akakujibu "unanisema mimi narudi saa nane za usiku mbona wewe baba yako anarudi saa nane za usiku ulishawahi kusikia mama yako anagombana na kumtukana bora mimi narudi nalala sianzishi ugomvi na kukupiga"...nadhani mmenielewa hayo na mengine mengi ambayo tunawaambia wanaume chuja ya kumwambia mwanaume asitafute fimbo ya kukuchapia..

0 comments:

Post a Comment