Monday, August 12, 2013

MWANAMKE: katika maisha wewe unanyota na baraka za kumuwashia au kumzimia mwanaume mwanga wake wa kuonekana katika dunia,hii haswa ni katika ndoa pindi mnapokaa zaidi ya mwaka pamoja katika nyumba moja na maisha yenu kuwa kitu kimoja, je hujawahi kumjua mtu ambaye alikuwa na maisha mazuri,kazi nzuri na hela mwanaume alikuwa ng'aring'ari lakini ghafla alivyomuoa msichana fulani nyota yake ikazima, akawa wa hovyo kabisa, kazi kafukuzwa, kama ni biashara haina faida mpaka anafunga, magari na nyumba anauza..na je umeshawahi kumuona mwanaume wa kawaida tu alikuwa anajimudu yeye tu lakini baada ya kumuoa msichana fulani sasa hivi anang'aa, anahela ana nyumba na magari..umeshawahi kuona vitu hivi..tambua wewe mwanamke ndio kiini kikuu katika maisha yako na mumeo uwezo wote unao wewe huku ukiomba kwa MUNGU azidi kuwasaidia...unapokuwa tayari kwa kuwa mke wa mtu muombe MUNGU akuandae ukawe nyota itakayong'aa na kila mtu akiiona apate kutambua uwepo wako katika maisha ya mumeo na kama wewe ni mke wa mtu na hukutambua umuhimu wa nyota yako basi muombe MUNGU akakung'arishe upya leo ukapate kuonekana.

0 comments:

Post a Comment