Friday, June 28, 2013

Katika Nyumba yako Mwanamke.........

kuna vitu ambavyo mwanamke hutakiwi kukosa katika nyumba yako nitaviongelea kwa mafumbo ili kujuwa undani zaidi basi wewe mwanamke usikose mafundo hayo jumapili ijayo 7/7/2013 na kila kitu kati ya nitakavyoandika hapa leo vitakuwepo siku hiyo.

Kwanza kabisa mwanake nyumbani kwako nilazima uwe na osheo la sufuria inahusu nini mwanamke ukasonga ugali na kushindwa kuosha sufuria ikabaki na ukoko, ni lazima uwe na kosheo tena sio kosheo tu linalomudu usafi bibi....

Pili mwanamke kwenye nyumba yako chupa ya chai muhimu, familia na wageni wako asubuhi au jioni lazima wanywe chai ya moto yenye ujotojoto haipendezi wala haina ladha mwanamke ukawatengea wageni chai iliyopoa.

Tatu mwanamke lazima uwe na fridge ya kuwekea maji jamani dar hii joto jingi mtu unataka ukirudi nyumbani wakati wote maji ya wepo unywe ukate kiu, na kiu ya dar kwa maji ya moto wala haikatiki ila kwa wale ambao hawawezi kunywa maji ya baridi basi hata ya moto pia ni sawa.

Nnne mwanamke lazima ndani kwako uwe na kabati tena zuri kwa ajili ya kuwekea nguo na lengine vyombo ili nyumba yako ipangike sio wageni tunakuja unakuta patupu mwanamke au kila kitu vuruguvurugu hujui hiki kipo wapi kile kimeenda wapi shoga yangu utaaibika.

Nimeonglea kikungwi zaidi na najuwa wengi sana watakuwa hawajaelewa ila kwakuwa utakuja kufundwa naamini utaelewa yote hayo, nimeandika hivyo kukata ukali wa maneno maana ni makubwa na mazito hayastahili kuandikwa hapa.

Lipia ticket yako mapema jumapili 7/7/2013 sio mbali na kumbuka mafundo haya ni kwa mwanamke yeyote anayejuwa yupo kwenye ndoa ama siku anajuwa atapata ndoa yake ili mradi tu uwe juu ya miaka 18 tunakukaribisha kiingilio 30000 kwanzia watu watatu tunakuletea tickets palepale majestic hall sinza kwa remmy kwanzia saa tano asubuhi mpaka saa kumi na mbili jioni...kwa kulipia tickets nipigie 0717 019320