Thursday, April 4, 2013

Kuhusu 26/4/2013...

Nataka muelewe kitu kimoja wapendwa kwa ambao wameshawahi kuja kufundwa wanajuwa utaratibu wetu tukiwa ukumbini ila kwa wewe unayekuja mgeni ni hivi siku hiyo hakuna picha zinazoruhusiwa kupigwa kinachofanyika humo kina baki humo hatuji pale kimaonyesho tunakuja kujifunza na sio kujifunza biashara ni mambo ya chumbani kwahiyo yanayofanyika pale ni ya watu wa zima na sio maonyesho jifunze beba unaloona linakufaa nenda kajipe raha wewe na mpenzio ambayo unaona ni makubwa kukuliko yaache palepale.

Wakati mwengine watu wanaocheza style za chumbani wana style mpaka watu wanapiga mayowe na mara nyengine nguo huwatoka kwahiyo kama unajijuwa wewe ni mtoto naomba usije ukatuharibia shughuli kwa kutupigia kelele..

Shughuli hii kwa mwaka tunaifanya mara mbili mwezi wa nne na wa kumi na mbili na makungwi wazoefu wanaojuwa kutufunda haswa kwahiyo ukikosa hii utasubiri MUNGU akipenda mwezi wa kumi na mbili labda tu kwa wale wanaotaka kufundwa private na wao pia mnakuja kwa appointment kumbukeni na bei yenu ni tofauti tuna makungwi wengi na wazoefu unanipigia tunakupa appointment yako.

Kwa maharusi watarajiwa wanaume kwa wanawake pia huwa tunawafunda siku tatu mpaka tano ili mkahimili ndoa zenu, na kwa wanaume ambao mpo humu msiache kuwaambia wanawake zetu waje nao ili nanyi mpate kufurahia mafundo ya hiki kijiwe chenu.

Mwaka jana niliamua kuanzisha hichi kitu ili sote tupate kujifunza na kufurahia mzunguko maana wengi hawapendi kwenda zaidi ya mara moja lakini namshukuru MUNGU wengi mmenipigia tokea mmeanza kufundwa mnajimudu na mnafurahia mzunguko.

Hii sio biashara na tuna idadi yetu ya watu kuingia hatujazi watu kwa kutengeneza pesa tunataka darasa ambalo makungwi wanaweza kulimudu, mkafundwa wote makaelewa na huku mkipata burudani mbalimbali ndio maana kila mara nawakumbusha kulipia mapema ikifika idadi tuliojiwekea hatutapokea tena watu mpaka mwezi wa kumi na mbili.

Lipia nafasi yako sasa nipigie 0717 019320 ulipie na kupewa dera lako kumbukeni zimebaki wiki mbili tu...

0 comments:

Post a Comment