Monday, March 11, 2013

Uswahilini kwetu..

MMhhh hapa aisee kweli nimeamini kama duniani kuna uchafu tena uchafu wa hali ya juu uswahilini kwetu jana walikuwa wanamsuta mtu kwa tabia yake chafu ya kulala na kaka zake..

Kweli kabisa mwanamke umezunguka kote ukakosa mwanaume mpaka ukaamua kulala na kaka zako tuliposhangaa kuna mtu akatokea akasema unamshangaa huyo tabia yake ya kulala na kaka zake mbona yule fulani wa mtaa wa nyuma analala na baba yake!!!!! yani wewe ukaikatikie mboo iliyokeleta duniani si unawazimu.

Inahusu nini sasa kumfanya mama yako mke mwenzio kisa nini hela, halafu mwanamke nasikia kakolea hana hata wasiwasi..anyways back to my point huyu shoga anatabia ya kulala na kaka zake mara ya kwanza ilipogundulika wazazi wake walimfukuza nyumbani kwa hasira na kaka mtu akahama wakaenda kupanga mbali na kwao wakaanza kukaa kama mtu na mume wanapika na kupakuwa pamoja.

Wakaendelea hivyo kwa muda ila kwa bahati nzuri ama mbaya yule kijana akahamishwa kikazi mkoa mwengine ndio kuachana kwao japo walikuwa wanawasiliana na kutumiana hela za matumizi baadaye huyu kaka hukohuko alipoamishiwa akapata mchumba ndio kuoa na kuanza familia.

Lakini huyu mwanamke hulka yake haikuhishia hapo na ninchoshangaa inakuwaje na hao kaka zake nao wanakubali!!! ama ndio ile hata ndugu yako akijilengesha unakula hakuna haramu!!! hapa aisee itakuwa ngumu tena namuomba MUNGU hilo jambo linipitie huko kwanza naanzaje au kaka zangu wanaanzaje kunitamkia kitu kama hicho..uuwii naona na undugu utakufa siku hiyo

Basi shoga yule kaanza uhusiano na kaka yake mwengine na sasa wanafamilia wamemchoka na kuanza kumfanyia vurugu na kumtukana na kumlaani sisi kwetu uswahilini nyumba zimebanana kama mkungu wa ndizi ukibwabwaja kwa nguvu jirani yako analo, basi ndio ndugu kuanza kumsema shosti sauti zikapaa zikawafikia wanakijiji wakajikusanya ndio mpaka tukajaa kusikia huo mkasa.

Shoga hata aibu hana wala hata kumuacha kaka yake kasema hamuachi na asiyetaka undugu na yeye wauvunje..hehe heiya umesikia hilo zoho likaendelea miye sikuona cha kuendelea kusikiliza kama wao kuachana hawataki siye wapembeni kinatuhusu nini kama wanaona imara kuwa pamoja wazae na mdogo wao maana mtoto wao atakuwa nani??????? 

Hili ndio jiji ukija na jembe utalima lami. 

1 comments:

  1. Evil spirits, we don't fight flesh but the spirit beings who have blind folded us.

    ReplyDelete