Thursday, December 27, 2012

Kuvunja laana ya kitovu..

Najuwa kuna wamama wakwe wanamatatizo jamani lakini kwa upande mwengine hebu tuangalie tabu walizopata mpaka wakatutunzia hawa wame zetu leo tunaojitapa nao, kama tunavyojuwa ya kwamba unapozaa mtoto wa kiume hulali usingizi wiki nzima ya kwanza mpaka kitovu kimedondoka, maana unabaki unaangalia tu kile kitovu kisije dondokea kwenye uume wa mtoto na baadaye kumpa matatizo ya kutoutumia vyema uume wake.

Ikitokea kama mtoto wako amedondokewa na kitovu katika uume unajuwa cha kufanya wewe kama mama ama kama unamjuwa mama ambaye mwanaye kimemtokea hivyo unajuwa la kumshauri?

Juzi alikuja mama mkwe wangu (mama mkubwa wa mume wangu)  kwangu katika story nyingi sana tulizopiga za kuhusu maisha na jinsi wao zamani walivyoishi katika ndoa zao ikatokea tukagusia hilo swala mimi nikataka kujuwa kama kuna ukweli wa hilo swala na akaniambi ni kweli kabisa na yeye kuna mama ambaye ni ndugu yao anamjuwa mwanaye alidondokewa na kitovu umeni mpaka leo mzunguko hafanyi na kuzaa hajazaa wala hajaoa kwasababu kila mwanamke anayekuwa naye anamuacha hashughuliki kuna mwanamke anataka mwanaume wa hivyo.

Nikamuuliza ameshahangaika kwa tiba hospitalini ama kunywa dawa za kienyeji akaniambia ile haina tiba za namana hiyo mwanangu tiba yake no moja ambayo inawashinda wa mama wengi hata mama yake na yule kijana pia ilimshinda ndio maana yupo hivyo mpaka leo nikazodo kumdadisi kwanini na tiba yake inakuwaje???

Akaniambia tiba yake inafanya kazi mpaka kijana awe amekuwa na ameshajuwa mwanamke yupo vipi  kwahiyo bila kumwambia wewe mama mzazi unatakiwa uende chumbani kwako uvue nguo zako zote na ukae kitandani kama unamngoja baba aje akupe mzunguko ukiwa umelalia mgongo  ukiwa huna nguo kabisa umuite mtoto wako huyo wa kiume chumbani atakapokuja na kukuona ukeni akashtuka basi atashtuka moja kwa moja mpaka kwenye uume na ndio hapo ataanza kufanya kazi kama wanaume wengine.

Kwahiyo akishastuka tu unaamka unavaa nguo usibaki bila nguo tena mbele yake kwa muda tena akishtuka tu basi, kwahiyo mama wa yule ndugu yake yeye alisema kuliko mtoto wake aone alipotokea bora abaki hivyo ndio maana mpaka leo yupo vile.

Inasikitisha kwakweli lakini pia inahitaji moyo kufanya hiyo tiba wangapi wangeweza?? mimi kama inenitokea hivyo sitowaficha ningefanya ili mwanangu apone dunia ya sasa hivi heshima uume pesa nyongeza kama mwanaume hujui kujitumia vizuri unatupwa huko kwenye dustbin kwani ulisikia yeye kwao hali, havai, halali ndio maana kaja kwako???? kafwata heshima ya mwanaume huyo..

0 comments:

Post a Comment