Thursday, August 2, 2012

Chezeya kuwekwa ndani weye..hehe heiya tajibeba

Ukitaka kunirusha roho rusha roho yako kwanza, ukitaka kuniteta miye anza yako kwanza..

Na usijitutumie eti unanikomoa achana na miye bibi roho nitakupaisha, ujute kunifahamu..ujuwe unanichefua uache kimbele front.

Kichwa kama kikaango naona wanichekesha sura kama jibwa koko tulio usiye na haya..

wewe kutwa unauza hususani kwa macheni na bei unapunguza sasa kwa shillingi ten..halooooo huna la kunitambua wewe bambucha nakujuwa lugha yako naijuwa mpaka inyeshe mvua, mafuta yako vioja hadi ule vitumbua...nyauba weee

5 comments:

  1. shost hebu punguza uswahili nawe cku hizi umekua mswahili sana!

    ReplyDelete
  2. mbn komment yangu umeibania bt frankly speaking punguza uswazi bwana wala hufananii!

    ReplyDelete
  3. chezeeeya utamu wa taarab, bibi kula raha upendavyo, maisha yenyewe mafupi, kama we unaona uswahili nenda kwa wazungu!!! tuache sie waswahili, mimi ni mswahili and am proud to be one.
    comment hazibaniwi hapa, hatuoni noma yoyote we comment zote zitarushwaaa, mwanamke kujiamini!!!

    kukwekwa ndani rose si mchezo, kinawasugua wasokonyola nakwambia, karibu watazikwa na roho zao mbaya, mke halali wa mnyalu mie aaaah napewa raha, kazi kwao.

    ReplyDelete
  4. Uswahili ndio mambo yote mnaukandia lakini uswahilini hambanduki. Sasa tukiwa wote wazungu kutanoga kweli aah Rosemary nimekupendaje mie achana na hao wazungu pori hawajujui hawajitambui; wakienda kwa wazungu halisi wazungu wenyewe wanawaota ni niggazz tu wakija huku ndio wanabana pua uswahili tu!

    ReplyDelete