Monday, June 7, 2010

HII NI KWA MAWIFI....

jamani hii ni kwa mawifi hata mimi nikiwa mmoja wao, hivi ni kwanini mafiwi huwa watu wa kwanza kuwaletea wake wa kakak zenu matatizo na maneno kibao?
nadhani mtakubaliana nami kwamba mtakuwa mmeshaona nyumba inavyoingiliwa na mawifi na maneno yao kibao mara huyu mwanamke wa kaka kwanza sio mzuri, wengine husema labda anajidai, anamashauzi ama wengine husema labda anamroga kaka yetu ndio maana sikuhizi kaka yetu huwa hatusikilizi sana..
hii nataka mawifi waelewe sasa wewe unajua kaka yako kapendea nini kwahuyo mke wake mpaka mumseme, haya hatakama sio mzuri kwenu yeye ndio kashazimikia mzigo pale na kuoa kama vipi simngeolewa nyie wenye sura nzuri? ama hata kama hana umbo zuri hilo umbo ndio lililomuweka kaka yenu roho juu mpaka akauchukua jumla..
mawifi jamani tuache maneno kwani hamjui kuna mambo mengine hakuna mtu anayeweza kumtatulia kaka yako kama sio huyo wifi yako, ama wewe leo kaka yako akitaka mtoto ukatayari akupe mambo umbebee huyo mtoto huh? muuendeleze ukooo.....
haipendezi jamani, tuwapende mawifi zetu kwa hali yeyote waliyokuwa nayo kwani na wao wanamapenzi mazuri kama kaka zetu kwetu...

0 comments:

Post a Comment