Monday, October 28, 2013

Neno hiloooooooooooo

Shalom
Kwanza nianze na vijana wa kiume. Misingi ya ndoa inaanzia kwenye mahusiano, lakini wakaka wengi siku hizi wamekuwa ni wavunja moyo sana. Ukijichunguza kwa makini utagundua ni wadada wengi sana umewavunja moyo na kuwaumiza. Unakuta kijana anaona ufahari kuwachumbia wadada zaidi ya mmoja na kisha kuwatosa, kuwachumbia na kuwatosa na wanapokuwa wanagombana kwa ajili yake anajiona kuwa ni mwanaume.

Leo unaona kama ni mchezo, na kweli wengi wanalia kwa ajili yako umewatosa baada ya kuwapa matumaini, lakini kumbuka apandacho mtu ndicho atakachovuna. Wasichana wanapolia kwa ajili yako umewatenda vibaya, maombi yao yanafika kwa Mungu na hakika atashuka kuwatetea. Kama huna mpango kwa kumuoa kwaninu kumdanganya na kumpa tumaini la uogo? Wengine mnawapanga makusudi kuangalia yupi bora, jamani mke sio bidhaa biblia inasema mke mwema mtu hupewa na Mungu. Acha kuwapanga wasichana badala yake nenda mbele za Mungu naye atakuonyesha yule mmoja ambaye ameandaliwa kwa ajili yako, aliye ubavu wako.


Imeandikwa na: Woman of Christ

0 comments:

Post a Comment