Tuesday, August 13, 2013

Thamani yako kwake...

Thamani yako kwa mpenzi wako unaijua siongelei na nyie wenye wapenzi wame za watu au wake za watu  kwakuwa huyo sio wako ni wa mwanamke na mwanaume  mwengine, ila wewe mwenye mumeo, mkeo au mpenzi ambaye sio wa kukopa unaijuwa thamani yako kwake, unapokuwa naye anakuaje, anakuitaje na anakuchukuliaje..anakupenda,anakuthamini, anataka kila mtu ajuwe wewe ni nani kwake au mkitoka kwenda sehemu anakaa tu kimya hata marafiki zake au watu wanaomjuwa wakimuona hakutambulishi kwa heshima..kama yupo hivyo hilo ni TATIZO lifanyie kazi lazima ujuwe thamani yako kwa mpenzi wako mimi mume wangu ananiita MALKIA na anamapenzi ya ajabu kwangu yani nikiwa naye sehemu mpaka mimi mwenyewe naona aibu kila mtu anayemjuwa atatambulishwa huyu ndio mke wangu, malkia wangu mama wa watoto wangu wawili hata tukiwa bar kuna bar ya jirani na kwangu kila mwanamke anamsifia na kumshangaa mume wangu ila sasa hivi walishamzoea utasikia tu huyo huyo kaoa bwana hakuna mwanaume aliyeoa mtaani zaidi yake maana yeye kutwa mkewe... je wewe unajuwa thamani yako kwa mumeo/mkeo/mpenzi wako...kila mwanadamu anamapungufu yake lakini ni vitu vizuri na vidogo kama hivi vinakufanya uzidi kumpenda na kutaka kuendelea kuwa na kusihi naye...

0 comments:

Post a Comment