Tuesday, August 27, 2013

Neno

1. Tuombe kwa ajili ya utii wa wake kwa waume zao. Kama wewe ni mke omba Mungu akuwezeshe kumtii mume wako hata kama ni ngumu. Omba neema ya Mungu na uwezo wa kuweza kumtii mume wako. Kama hujaolewa omba uweze kumtii mumeo siku ukiolewa. Mume muombee mke wako aweze kuwa mtii kwako.

1 PET. 3:1-2 
"Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno; wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu."

EFE. 5:22-23 
"Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili."

Source: Woman of Christ

0 comments:

Post a Comment