Wamekata kona wamekubali penalty..hehe heiya
Nimeanza na mizizi penzi si la mwaka jana hatukuingia juzijuzi jiji la Dar es Salaama, tumelipandia ngazi tukashusha na milima...
Full stop wote kimya...acheni kelele na siruhusa kujitetea, ole wenu mnaopita njia za panya kunifwatilia mimi ni komando wa kike halahala nitawalipua...
Tena nalipa bishosti wa ukweeehh na ninajuwa kunengua, kanipenda kanizimika kweli na haswa pale ninaporembua..haloooooooo
Sasa wezi wa mabwana nawaambia nitawachakachua, nawapa onyo full stop hii ni challenge full gear...
Nyie type zenu za vichochoroni ndio zinazowafaa sio wangu chumba na varanda tena ghorofani nampandia
Heri kuvaa kandambili kulio mdundo mbovu
Hapa kwangu mmechemka ninaladha tamu sana ndio maana hataki kutoka, hata mje na waganga lorry zima himaya yangu keshafika, mlilie mizimu na makafara na mchinje hata paka..haloooooo lako hilo
Allah unajitapa unalipa utafuti wako ukamuweka..wewe huwezi milki yangu baby cute wa kiafrica kwanza nipo peke yangu nimetulia na mume wangu mtoto wa uhakika..sweety jaffari ally mtoto wa kikwere..hehe heiya
POLE SANA KHADIJA KOPA...
Thursday, June 6, 2013
Khadija Kopa - Full Stop..chezea watu na wame zao weye....
12:57 AM
No comments
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment