Wednesday, March 27, 2013

Kwa WANAUME...

WANAUME..... kuweni makini sana mnapochagua Wanawake wa kuwapenda,ili wawe wake zenu.Wanawake wa siku hizi woteee wanataka ndoa,Vimeo wanaota ndoa,Virukanjia wanaforce ndoa kwa mimba za ghafla na kupitiliza siku zake,waungwana nao wanataka ndoa.
Wanawake wa siku hizi wako radhi wajiunge na Kwaya ili waku-impress wewe Mwanamaombi unayesali kupata mke mwema uingie kingi,na usipotulia magotini kuomba utajikuta umeoa mke feki...
Wanawake wa siku hizi hawaoni haya kujibadili tabia temporarily ili uwaone Wife Material,anakupa maji huku anapiga goti unajua umepata yule uliyemtarajia mwenye adabu na anayejitunza kumbe unaopoa guberi........
Kumbuka,Mke ni Waziri Mkuu Kivuli wa Serikali ya Familia yako,ukioa Waziri mkuu Kilaza Serikali yako itaangushwa na Waasi wachache kwa vita vya siku 2 tu Sali sana,Mke mwema hutoka kwa Bwana,sio Facebook wala kwa Kum-follow Twitter...MAPENDO......
 
 Source:Vijana wa katoliki Tanzania

0 comments:

Post a Comment