Thursday, March 7, 2013

Inahusu nini sasa???

Jamani hapa nimekerwa mpaka nasikia kichefuchefu yani hivi kwani hizi ndoa za kupangiwa na wazazi bado zipo jamani inahusu nini sasa kisa wewe mzazi wangu ndio unijuwe nataka nini kwa mwanaume mpaka unichagulie mume, jamani mume ama mke mtu anajichagulia mwenyewe, au ndio yale mambo ya mtoto wa fulani kasoma anakzai ya maana basi amuoe mtoto wangu..aihusu kabisa

Jana niliitwa sehemu na shoga yangu mmoja akawa ananihadithia kisa kimoja cha jirani yao, shoga naona na mimi nikaombe kazi sasa leo tena maana hizi habari za uswahilini zimenizidi, eti huyo jirani yeye alipangiwa ndoa na wazazi wake alikuwa anakaa mbeya kijana yupo dar es salaam akapelekewa picha ya kijana kwamba wazazi wa mwanaume wanataka yule dada aolewe na huyo mtoto wao.

Na wazazi wa mwanamke hawakukataa wakamwambia mwanamke na kumuonyesha picha na maneno kibao mazuri yule msichana tena kusikia bwana yupo dar inahusu bibi kutaka kuingia kwenye jiji hili akatae tena achekwe shoga akakubali na kukubali kuolewa basi shughuli za huko na kule mpaka ikafika siku ya kuolewa ilikuwa ni harusi tu hakuna sijui send off wala kufundwa kitchen party.

Mwali yule na wazazi na ndugu zake wakasafiri kuja dar kuolewa sasa siku ya ndoa shoga akataka kugoma kuolewa baada ya kumuona kijana mlemavu hana mkono mmoja inahusu nini??? angekuwa hana mboo kweli mkono inanihusu nini kama anaweza kunishika na mkono mmoja akanifikisha kileleni huo mwengine unanihusu nini...hehe heiya

Basi mwanamke ndio kutaka kugoma mama yake mpaka kalia akimuomba asimtie aibu shoga ndio kukubali kuolewa kwa shingo upande, lakini tokea kaolewa nyumba haina raha hampendi kabisa mumewe, yani anamfanyia vituko vingi sana hata kuongozana naye hataki yani anaishi tu kwavile hana pa kwenda, lakini bwana sijui ikawaje MUNGU mkubwa siku wakakutana kwenye sita kwa sita mama akabeba mimba, akazaa lakini bado akawa hampendi mumewe anamfanyia vituko yule baba anapika, anajifulia, wanagari moja ambalo yule baba hakuwa mchoyo kumfundisha mkewe kuendesha lakini yule mama ndio analiendesha yule baba anaenda kazini na daladala.

MUNGU akawajalia wakazaa mtoto wa pili hali bado ipo hivyohivyo sasa hivi wanamsichana wa kazi basi yue dada ndio anafanya kazi za yule mama, yule mama akabahatika kupata kazi basi kutwa anarudi saa sita za usiku anasingizia kazi yani nyumba haina raha sasa mama wa mwanaume ndio kaja kuona yale maisha ndio kuanzisha vurugumai ya kumtukana mwanamke ndio siri zikagundulika kama ndoa alipangiwa.

Ndugu mume na mke unajitafutia mwenyewe hata walemavu pia wanahaki ya kupendwa na kupata wa kuoa/kuolewa kama hana ulemavu kwenye mboo na anaweza kukufikisha, anahudumia nyumbani anakupenda kwakweli unataka nini kidonda cha moyo..utakufa nacho

0 comments:

Post a Comment