Tuesday, January 8, 2013

Weusi....

Leo wapendwa nataka kuongelea jambo ambalo linasumbua sana wanawake sio kwamba wanaume wao hawana bali hawalichukulii kiundani sana kama sisi wanawake linavyotusumbua, weusi katikati ya mapaja najuwa wanawake hapa wenye tatizo hili wamesema kweli kabisa..

Weusi huo wanawake tunao sana kwasababu ya jasho katikati ya mapaja maana kutwa yanagusana kwa kuvaa sana skirts na vitu vingine vingi vinavyofanya mapaja kuwa meusi labda hata mimi sivijui utafanyaje kama na wewe mapaja yako yapo hivyo..utatumia mafuta ya nazi

Ndio mafuta ya nazi ndio dawa ya kusafisha huo weusi ukishaoga asubuhi, mchana na jioni unayapaka kwenye mapaja ndani ya mwezi bila kuacha hata siku moja utaona huo weusi wote unapotea kabisa.

Kama hukulijuwa lako hilo beba na baba mpe na mkeo pia ukirudi nyumbani ..

0 comments:

Post a Comment