Tuesday, November 20, 2012

SOMO..

shoga habari yako, mzima weye na anyekupa usingizi je natumaini ni mzima kabisa shoga nakazia sana kuwapa somo wanawake kwakuwa siku yao ya kufundwa inakuja tukimaliza hapo tutarudi kuongela maswala ya mapenzi kwa ujumla na wanaume pia.

Shoga leo nataka tuongelee simu ya mkonono, ushanipata? eenhhee ndio simu ya mkononi ndugu kila mtu haswa kila mwanamke ana simu ya mkononi shoga za kila aina, kila rangi na kila size sasa shoga kama wewe simu yako inamatatizo inahusu nini kumwambia shoga yako siupeleke kwa fundi!!!!

Oooh simu yangu desplay imekufa, sijui button zimetoka mara siwezi kuandika message vizuri inahusu nini kuifanyia matangazo siutengeneze mueleze fundi aitengeneze shoga mara huyo shoga yako unayemumbia tatizo la simu akaichukuwa akaenda kuitengeneza yeye ikapona akaichukuwa moja kwa moja utafanyaje???

Jibu unalo mwenyewe au nimekuacha????? shoga hiyo njia ata sipiti siyo huko twende kulee tukutane 7/12/2012 tukujuze zaidi kuhusu hili swala..kama nimekupoteza niwie radhi..ila shoga hapa mjini ukija na jembe utalima lami.

0 comments:

Post a Comment