Friday, November 16, 2012

SOMO..

Shoga upo? shoga najuwa wewe kupika unajuwa tena naamini chakula chako kitamu ndio maana shemeji namuona anazidi kunawiri chezea weye..

Shoga sasa leo tuongelee ule mwiko siunajuwa baada ya kupika haswa ugali mwiko unakuwa mchafu, shoga miye nikisonga ugali wangu mwiko ndio kitu cha kwanza kukiosha halafu sufuria baada ya hapo wewe je?? shoga kuna kila aina ya miko kwanza unalitambua, shoga usije kutumia mwiko wa wali kwenye ugali utaumbuka maana nyonga yake sio ya kitoto..halooooooooo ulikuwa hujui shaurilo

Shoga mwiko ndio ushasongea mwiko hujaosha umeganda unafanyaje unauloeka ama unausugua na kijiko..hehe heiya shoga unautia doa unavyousugua na kijiko unaharibu muonekano wake jamani...sasa utaufanyaje na ndo ushaganda....NIMEKUACHA GEUZA BWANA SIO HUKO UENDAPO SHOSTI...

Haloo shoga number moja ndio miye, pili miye mwenyewe na tatu pia miye..tukutane 7/12/2012 shoga ntakurusha roho wewe ukitoka hapo ukasimulie waulize wenzio wanaojuwa kazi yetu..hehe heiya lipia nafasi yako sasa 

0 comments:

Post a Comment