Thursday, November 1, 2012

Hehe heiya Mfamaji weye?????????????Chezea waswahili siye

 Husda na roho yako ya chuki ya chuki imekuweka pabaya kutwa mdomoni wako sitoki waniombea mabaya, ila rabi yu pamoja nami yamkini sina chuki nawe wanitangazia ubaya kwa watu..

Kama kupewa mimi amenipa MUNGU nakuchukuwa pia atachukuwa MUNGU, madhali hajaamua huwezi kumuingilia MUNGU na nilichojaaliwa ndio kitakuwa changu..tapa tapa endelea maji yanywe kwa uchungu wewe mfamaji mwenzangu.

Nirehema ya MUNGU japo ukiwa hutaki endelea na majungu..kutwa maneno mfamaji unayatoa na minong'ono ukiona naendelea kwenye vinono usione nimesogea watoa chano yangu yasiwe sawia..

Vifunike vyote vyano bure ndambi wajitia utaumiza mkono ukuta ukijipigia..hehe heiya maji ya shingo watapatapa mfamaji funga vibwengo hauokoki kwenye maji...endelea na majungu

Uso unanikunjia kila unaponiona na mabaya kunidhulia, najuwa kinachokuuma ni yangu mafanikio mimi ndio nimeshasimama wewe kachunge chungio..chezea miyeeeeeeeeeeee


0 comments:

Post a Comment