Tuesday, October 23, 2012

Mama Mkwe weeee...

Natumai mzima da rose, mi ni mwanamke nimeolewa na ndoa yangu nw inamiezi kumi yaan ni uvumilivu ndo ulinifanya nifikishe hyo miezi,mamkwe wangu na wifi yangu kila kukicha wanamwambia maneno mume wng mara mkeo hakufai,kuna kipindi tulienda dar kikaz kama wik 2 tukafikia kwake basi ikifika mida ya mwanae kurudi ananuna na akifika anamwambia maneno basi mume wng ananiita mbele yake ananisema ye ndo anafurahi,kuna siku tulikuwa tunataka kutoka out mume wng nilimuandalia mchemsho wa samak sasa m na yeye tumeshazoea ye huwa anakula kichwa m mkia sasa m nikaenda chumbani mara moja yaan mamkwe akamwambia haiwezekan ye ale kichwa yaan nilichambwa hatar yaan kwa hasira out yenyewe sikwenda ,kesho yake mume wng hakwenda kazin akaenda mjin akaniletea BB na kunitoa out kama samahani, tulivyorudi yule bibi kuiona akamwambia mwanae anachezea hela yaan mume wng alimchamba na akamwambia asiingilie ndoa yetu tena lakin hakomi, kuna siku alikuwa anamwambia wifi yangu kuwa alimwambia mwanae acnioe hakuckia sasa atanikomesha ntaondoka mwenyewe,ebu nishaurin mana c tunakaa mkoani lakin kila cku cm haziishi kwa mwanae kumpa maneno.

3 comments:

  1. duh pole bi dada jikazw tu na kumuomba mungu sana na shukuru mungu mume anakupenda na amsikilizi mama ake!ala usjl zidisha mapenzi na weka masikio pamba ck zinaenda.

    ReplyDelete
  2. HA HA HAAAAAAAAAA HUYO MA MKWE ANGEKUWA NDO MA MKWE WANGU ANGEJUTA KWA NINI NILIOLEWA NA MWANAE PIA MM MUME WANGU NIKIMPA SAMAKI AU NYAMA ANATOA MINOFU KARIBU YOTE NA KUNILISHA THEN ANAKULA ALIVYOBAKIZA NA HII SI NYUMBAN HATA HOTEL AU KWENYE SHERHE KIAC KWAMBA HUWA NAONA AIBU SOMETIMES BUT NDO MTINDO WAKE WA MAISHA, SO MAMA MKWE WAKO NOMA ANAINGILIA MTINDO WA MAISHA YENU MPOTEZEE HUYO.
    USHAURI: JARIBUNI KUTOFIKIA KWAKE MWENDE TU KUMSALIMIA NA KUONDOKA KUEPUSHA LAWAMA

    ReplyDelete
  3. Bi dada hizo ni kelele za chura hazimnyimi ng'ombe kunywa maji,ucwajali kaza buti

    ReplyDelete