Wednesday, August 22, 2012

Chezea Gusa Gusa wewe..

Kuna dada mmoja hivi yupo kwenye ndoa mwaka wa sita huu sasa, lakini hana amani na ndoa yake yani na amani inavunjika kwa sababu ya mumewe kupenda mechi za nje, yani yeye anasema ni mwaka wa mwanzo tu ndio alikuwa na furaha na ndoa yake lakini sasa kila kukicha wananuniana na maugomvi kibao kwenye nyumba.

Alishawekewa vikao vingi sana na familia mumewe akiahidi kwamba atajirekebisha lakini ikawa kila kukicha afadhali ya jana, ikafika kipindi akataka kabisa aondoke yani aachane na mumewe lakini ananiambia kuna siku moja akiwa tu peke yake ndani akajiuliza nikiondoka sitowatendea haki watoto wangu kukuzwa bila mapenzi ya baba nitakaa tu na mume wangu akirudi niongee naye anieleze sababu haswa zinazomfanya kuendekeza umalaya labda kunajambo ambalo kila siku alikuwa naogopa kulisema kwenye vikao tunavyokaa kuzungumzia matatizo ya ndoa yetu.

Jumamosi moja akaamua kulitoa dukuduku lake na kuongea na mumewe, mumewe akamwambia kwamba umalaya wake unasababishwa na yeye mkewe, kwamba yeye hataki kumpa nyuma na huko anapoenda huwa anapewa nyuma!!!!!! kwahiyo kuliko kumlazimisha ni afadhali tu awe anapata huko nje.

Mkewe kwasababu alikuwa anampenda sana mumewe na hakupenda amani inavyovurugika katika nyumba yake  akaona kama sababu inayomtoa mumewe nje ni upande wa pili basi atampa mumewe upande wa pili!!!!!!!!!!!!!!!!!!hehe heiya

Kweli shosti anasema akaanza kumpa mumewe upande wa pili japo iliuma lakini alijikaza na baada ya muda akazoea na akaniambia kweli mabadiliko yalionekana kwenye ndoa mwanaume alibadilika, kukawa na amani yani alifurahia sana ndoa yake mpaka akawa anajilaumu kwanini hakumpa tokea zamani.

Muda ukaenda maumbile ya shosti sasa yakaanza kuharibika, pakatanuka ikafikia mpaka sasa akiwa ameketi akisimama anakuwa ameloa nyuma, yani akitoka ni lazima avae pedi ili asiumbuke barabarani!!!! ilipofikia hapo mumewe akaanza tena tabia yake ya zamani ya kutoka nje, mkewe akimuuliza kwanini ameanza tena na huku yeye anampa mumewe humwambia kwake kumesha tanuka anatafuta vilivyo sinjaa!!!!!

Yule dada anasema alitaka kufa, ameharibika kwa kumpa raha mumewe sasa mwanaume bado anamtesa kwa umalaya, yani kwa jinsi anavyomchukia mumewe sasa anataka hata kumfanyaje sijui, sasa amebaki kuishi maisha ya utumwa tu amani hamna wanaishi kimazoea tu maana mwanaume kama kala miguu ya kuku kila kukicha mguu na njia na dogodogo.

Na sio kwamba ni anamwanamke mmoja kwahiyo duh huyu kaka noma yani yeye anakula mbele na upande wa nyuma na kwajinsi mkewe alivyonihadithia ameshawapakuwa  wanawake wengi sana!!! 
dunia hii mmhhhh


7 comments:

  1. mwanamke kwake ni wapi jaman, a very sad story DUuuuuuuuuuuuh, nipo hoi

    ReplyDelete
  2. Mh!! mwenyezi mungu atunusuru

    Zaituni

    ReplyDelete
  3. awe mwangalifu na watoto wake, wasije kufata tabia ya baba yao. ukila vya wenzio na vyako huliwa.

    ReplyDelete
  4. eeeeh jamani hii inatisha, lakini wanawake pia tuwe tunachuja mambo mengine na tuwe na msimamo, haimaanishi kumpa raha mumeo ndo mpaka umkufuru mungu wako na kujidhalilisha. huu ni uchafu na madhara yae yanajulikana, ni kweli huyu dada alikua anataka kunusuru ndoa yake, na kwa hilo alikua jasiri, ila tuwe tunatizama mbele na kujitahidi sana kutokumkufuru muumba wetu na kijipenda sisi wenyewe. Tendo la ndoa ni wote kufurahia na kuridhiana, halina maana kama unafanya kumridhisha tu mwenzio wewe huku rohoni unasononeka.

    ReplyDelete
  5. Ya leo kali, makubwa madogo yana nafuu, mapenzi gani hayo jamani wanawake wenzangu? Mapenzi ni kujipenda wewe mwenyewe kwanza na kufanya lile ambalo lina manufaa kwa afya yako. Hivi hamjasikia kuwa ukimwi uliwamaliza magay wengi? Huko nyuma ni rahisi sana kuambukizana maradhi, yaani namuonea huruma huyo dada atakuwa anaishi na Lucifer aliye kwenye umbo la kibinadamu.

    Kuna kaka mmoja nilikuwa nafanya nae kazi yaani yeye ngono kwake ilikuwa kuliko chakula hata muda wa kazi alikuwa anatoroka anaenda kwenye madanguro. Kumbe virusi vilikuwa vinamfanya ajisikie kufanya ngono muda wote. Na alikuwa anawapata hasa!!

    ReplyDelete
  6. Mmmhhhhhhhhhhhh hii nayo ya karne dada wanamme hawabebeki usijidanganye.POLE KWA YALOKUFIKA.
    USHAURI WA BURE: KAMA UNAMTOTO WA KIKE HAKIKISHA UNAMFUNDISHA UBAYA WA KUTOA TIGO ASIJE DHURIKA MAANA HIMSTORIA HUWA INAJIRUDIA ISIJE IKAJIRUDIA KWA BINTIYO

    ReplyDelete
  7. Jamani wanawake tujipende, mwanaume kama ni malaya ni malaya tu. Badala ya kumlilia Mungu aingilie kati katika ndoa, unaamua kumkufuru.

    Mungu husikia, we just need to be patient and listen to what he has to say to us.Hajachelewa amlilie Mungu katika hili.

    ReplyDelete