Thursday, April 12, 2012

SOMO......

Jamani wapendwa haswa wale wa kina miye leo nataka niwadokeze jambo unazijuwa kashata za kungu wewe? unazitumia ama hujawahi zitumia?

Shoga nitakueleza kashata za kungu zinautamu wake japo kwa ladha ni chungu, kwanza kashata hizi kazi yake ya kwanza ni kukupa raha ya kutizamwa ushanifahamu? yani mwanamke raha mtoto wa kike jicho litizamwe jicho ukilifungua linalegea na kuita sio wewe mpenzi wako hata siku moja hajawahi ona jicho linaaibu kila siku unamkazia mtoto wa watu jicho ka umelamba ndimu...wala haihusu

Pili kwa wale ambao huwa hawanahamu ya sita kwa sita yani hapa hizi nazo hucheza kaa dawa, ukila wewe kashata zako tatu tu aka raha muhstarehe mwenyewe bashasha zinapanda uanze tafuta simu na kumpigia huyo mumeo na usile hizi kama unajuwa mpenzi yupo mbali hatawahi kukupa dozi maana zitakutesa wewe...usiombe

Nadhani kwa wewe ambaye ulikuwa unalalamika hamu huna ya kumpa mtoto wa watu chakula chake cha usiku sasa utakuwa umenipata na kunielewa si ndio mamii...kazi kwako sasa

1 comments:

  1. Mumy nazihitaji saaaana hizi..napata wapi?

    ReplyDelete