Thursday, March 15, 2012

YANI HAJALI NA WALA HATAKI KUELEWA..

Dada mimi ninalangu rohoni ambalo nimeliweka kwa muda mrefu sasa naogopa nisije kufa nimeamua kulitoa ili nipate ushauri kutoka kwako na kwa wenzangu wote wa humu.

Nimepata mwanaume dada nipo naye mwezi wa tano sasa, ndio nampenda na ananijali sana lakini tatizo ni moja ambalo nimeliona kwake na kujuwa nisipo tafuta utatuzi mapema inaweza kunicost baadae.

Mpenzi wangu game yake kitandani ni nzuri sifa zake ninampa kwakweli lakini jamaa ni mchafu sana hata kama wanasema mapenzi ni machafu lakini uchafu huu naona kama siwezi tena kuuvumilia, yani kijana ni kwamba hata kama nikiwa kwenye hedhi jamaa bado anataka nimpe mamboz, mara ya kwanza nilikataa nikamueleza tatizo kwamba asubiri mpaka nikimaliza lakini hakutaka mpaka tukaishia ku do.

Mwezi wa tatu tena ikatokea nipo kwenye hedhi jamaa akaomba tena mzigo baada ya kumuelewesha kwamba haita wezekana kwasababu nina bleed, lakini akaniambia hajali lolote hiyo bleed yangu kwani inaziba ishu yake isiingie?????? kwakweli nilikasirika basi tu kwa vile ndio mwanaume wangu naogopa kutemwa kwa kisingizio nimemnyima chini.

Swali langu ni kwamba je ninaweza pata matatizo gani nikiwa nampa huku na bleed? na kwa wanaume kwani kuna raha gani unayoipata mpaka mtu anakataa na kushindwa kunivumilia mpaka nimalize hedhi?

1 comments:

  1. angalia asije pata magonjwa kwa sababu ile damu ni uchafu.

    ReplyDelete