Tuesday, May 31, 2011

UNAJUWA KAMA MWANAUME NI SUFURIA NI RAHISI KUPATA MOTO?????



jana nilikuwa na rafiki yangu tukawa tunaongea akaniambia jambo moja ambalo lilinishangaza yeye na mpenzi wake wamekuwa pamoja mwaka wa tatu sasa na ukiwaona jamani mapenzi motomoto mpaka mimi huwa nawaonea wivu sana lakini jana akaniambia kitu ambachi kilinishangaza sana akasema kwamba yeye tokea awe na huyo kaka hamna hata siku moja ambayo alifika kilele na hata kama ipo basi ni siku nyingi sana hata hakumbuki ladha yake...


kwakweli kwangu nilishtuka sio kwa vibaya ila kaka alivyokuwa mtanashati sikujuwa ya kwamba hawezi kumfikisha mke wake kileleni hapo ndipo tulipogundua mwanamme kweli yeye ni sufuria anasema yani akiingia tu dakika tatu ameshamaliza kwakweli hata ingekuwa mimi ningekasirika yani hapo wewe mwanamke hata bado hujavuta hisia vizuri ya kupanda mlima huku mwenzako ameshafika...duh!!!!




jamani wanaume muelewe ya kwamba mwanamke ni kama chungu kinachukua muda sana kukamata moto na kikikamata moto mpaka upoe shughuli ni kubwa basi jifunzeni kwenye raha usifike kilele kabla ya mwanamke wako jitahidi ukisikia vinataka kutoka waza hata kitu chengine ghafla ili usimkatishe mwenzio..... usije ukasaidiwa na wanaojuwa kumfikisha utajitia aibu

3 comments:

  1. Haya mambo haya kwa kweli ni shughuli kweli...mwanamke anahitaji kuandaliwa kwanza sio kuja tu na kutoka..Kaaazi kwelikweli.

    ReplyDelete
  2. Kila kitu kinahitaji somo na mafunzo. Ila somo la shughuli hii ni la MAISHA!!!! Haliishi!!!! Kila mmoja wetu ahitaji kuchimba na kutafiti kila siku kuiboresha hiyo SHUGHULI!!!! Na siyo wanaume tu; hata wanawake pia. Wapo wengi wasiojua kuridhisha pia!

    ReplyDelete
  3. Kila kitu duniani kinahitaji kujifunza, kukijua ikiwezekana hata kukisomea. Lakini katika yote hili ndilo kiini cha kusoma, kufanya kazi, kutafuta pesa, kuiba, kuvaa vizuri; ili mradi ulipate na kuliridhia. Uwe mwanaume au mwanaume yakubidi ulielewe somo hili fika. Na sio wanaume tu tunaohitaji kujua kuridhisha; hata wanawake vile vile...Ikiwa mathalan, jamaa "anachanua" haraka; basi wewe mwanamke yakubidi ujue namna ya kumfundisha somo. Hii si kazi ya lipua lipua, ushindani au kubabaisha; yahitaji kuchimba, tena kuchimba maisha yako yote. Kuna mwanamuziki mmoja wa zamani marehemu James Mpungo aliwahi kuniambia kimasihara kwamba ngono (na mapenzi) ni kama sukari; haiiishi utamu. Ni utamu wa daima...

    ReplyDelete