Monday, May 9, 2011

MWANAMKE KUMTONGOZA MWANAUME NI SAWA????

tumezoea ya kwamba mwanaume ndiye mshikadau kwenye mapenzi ya kwamba yeye ndiye anayetakiwa kumwaga sera pale anapokiona akipendacho (mwanamke) hiyo sawa...


lakini je inakuwaje kwa wale wanaume ambao kwakweli sijui ni aibu ama kutojiamini hawezi kabisa kutongoza mwanamke na je kama mwanamke naye ametokea kumpenda huyu kijana ni vibaya yeye kuanza kumwambia ili kumrahisishia huyo kaka???????


ama hapa ndio pale mwanamke unapoonekana muhuni unatabia mbaya ukianza kumwambia mwanaume unavyojisikia, ama nyie wanaume mwanamke anapokuambia kama anakupenda mnapokubaliana baadae mkigombana ndiyo inakuwa fimbo ya kumchapia?????


kwahiyo tunalichukuliaje ni sawa sio uhuni?

2 comments:

  1. Kwa mila za kiafrica, kumtongoza mwanaume kwakweli haiwi nzuri, wengi watakukimbia baadae. Ulaya kumtongoza mwanaume ni kawaida. Sasa sijui kama huyo mwanaume alishakaa ulaya au bado, maana anaweza kuona hicho ni kitu cha kawaida. Mwanaume wa kiafrica baadae mkikorofishana tu atakwambia kuwa ni wewe ndio ulimfwata!

    ReplyDelete
  2. Kwa desturi yetu ya kiafrika mwanamke kumtokea mwanaume sio kitu kizuri tena hakipendezi,ila wa wenzetu wa ulaya ni jambo la kawaida hata km itatokea kuacha hakuna hatakee msema mwenzie. Ila kwetu hata kabla ya kuacha ataaacha kutafuta sifa kwa marafiki zake kama ulimtongoza,siku mkiacha ndio kabisa yatakuwa kama matangazo ya biashara. Tatizo ilikuwa hapo!!!!

    ReplyDelete