Friday, February 25, 2011

TABIA ZA KURITHIANA MUME AMA MKE JAMANI NI UUNGWANA?

nimeshangazwa kwamba bado mpaka leo kuna watu na makabila wanarithiana wake ama wame, jamani hata baada ya kupata maendeleo yote haya bado mila kama hizi zipo!!!!!!!

kuna baba mmoja kwa jina namuhifadhi yeye mkewe amefariki kama miaka miwili iliyopita kwa ufahamu wangu kama mkeo ama mumeo amefariki na ukajihisi unahitaji mtu wa kumaliza naye uzee sawa lakini asiwe ndugu wa huyo mkeo ama mumeo...

miaka miwili imepita ukweni kwa huyu baba wakamwambia sasa inabidi umrithi mdogo wa mke wako ili awe mkeo!!!!!!!!!!!!!!!!! japo ilikuwa ngumu sana kwa huyu jamaa lakini angefanya nini na familia imemkazia ikabidi amrithi mdogo wa mke wake....

tatizo likaja pale wanapokuwa chumbani huyu baba hana mapenzi kabisa kila anapokutana kimahaba na huyu dada anasema kutwa humfikiria marehemu mkewe, muda umeenda huyu dada mpaka akabeba ujauzito sasa ameshajifungua watoto watatu lakini mwanaume bado anahisi atashindwa kumchukulia kama mke wake....

anasema anajitahidi sana kumpenda kama alivyompenda mkewe lakini inakuwa ngumu inabidi tu aishi naye kuepuka lawama kutoka kwa familia mara nyengine anataka hata kukimbia nyumba pinsi yanapomzidi....

wewe mwenzangu unahisi anayofanya ni mema, hata kama hana mapenzi ya kweli kwa huyu mdogo wa mkewe unadhani aendelee tu kumvumilia kutunza heshima kwenye familia ama aondoke tu..

0 comments:

Post a Comment