Sunday, February 27, 2011

MSICHANA WANGU WA KAZI JAMANI SIJUI NI MCHAWI 2

jamani wapenzi kuna jambo nataka niliweke wazi kuhusu hiyo mada niliyoiandika mwanzo mama paulsen yeye hajaolewa alizaa tu kwahiyo anakaa yeye na msichana wake wa kazi huyo pamoja na mtoto wake aliyemzaa maana kuna comments nimeziona kwamba huyo msichana anaweza akawa amelala na mume wa mama paulsen ndio maana dharau hazimuishi...

najuwa tatizo kubwa kwenye nyumba kwa hawa wasichana wa kazi pindi wanapoanza dharau ni kuwa wamelala na wame zetu, wakati mwengine pindi mke wake akiwa kwenye ujauzito ndipo wanaume wengine huchukulia huu ndio wakati wa kula upande mwengine........

lakini naamini kwa mwanume anayempenda kwa dhati mke wake kama ni kutaka tendo landoa na mke wake hawezi kumpa basi kwa heshima japo siliungi mkono ni afadhali akale nje kuliko kula beki tatu, ambaye ameletwa na mkeo na mkeo huyohuyo ndiye anayemlipa, kumlisha, na kumtibia wakati anaumwa....

hiyo ni dharau kubwa sana kina baba mnaweka kwa wake zenu...

0 comments:

Post a Comment