Tuesday, September 14, 2010

JAPO NINA MUME NASHINDWA KUACHA KUJIUZA...



nimeolewa jamani nina miezi saba sasa, mume wangu huyu tulikutana kwenye bar ndipo akanipenda na kunisihi niachanne na kujiuza akiahidi atanisaidia kwa kila kitu..
nikakubali na kuwa naye na tukafunga pingu za maisha, mume wangu huyu kwa kweli sijutii kuolewa naye ila tatizo ni moja nashindwa kabisa kuacha kwenda kuonana na wateja zangu wa zamani na haswa wale waliokuwa wananipa hela nyingi.
mume wangu hela ananipa lakini sio nyingi kama ninazopata kwa siku kwa wateja zangu fulani, hajui wala hajawahi kunihisi kama najiuza tena, nifanyaje kabla hajagundua jamani na huku nimeshanogewa?

5 comments:

  1. mmmmmmmmmmmmhhh nafkiri haupo serious na ndoa means upo staki nataka na alwayz mshika mawili moja humponyoka,kwanza rithika na ujue mpaka umeolewa huyo kk alikupenda na ivyo kua na heshima,tabia ni mazoea jaribu kua karibu na mume wako na kata mazoea na hao wateja wako kwani usipopatikana nao hawatakutafuta chanzo ni ww!na ufocus mbele kua kuna magonjwa wote ww na mumeo kama mmeamua kuoana tulieni maisha si kwa kutangatanga kama ndege.

    ReplyDelete
  2. we sasa una pepo aisee inabidi uombewe kama huwezi kuomba mwenyewe, labda nikuulize kwani huyo mmeo hakufikishi kileleni?au je hakupi mapenzi?sasa kama mapenzi anakupa na unaridhika pia anakuonyesha furaha ni nini unahangaika?unataka umletee ukimwi?mi ninavyojua hali yoyote uliyonayo mtu ambayo unaamini kuwa huwezi kuacha au kutoka ni wewe mwenyewe kwa kifupi we umeathirika kiasikolojia na si vinginevyo pia mazoea ndo yanayokusonga zaidi, ila mtu ukiamua kubadilika na kuacha inawezekana ila tu wewe umeshupaza tu shingo yako na itavunjika, jamani kaa utafakari we unadhani hizo hela unazopewa zimeshakufikisha wapi hadi sasa?si bado unagundua hazikutoshi?kwahiyo ndo ujue kuwa sio issue ila unahangaika na ulimwengu na ya wezekana huko mbele yakakupata ya kukupata tena makubwa zaidi, asiee acha na umeuheshimu mmeo kama ulimkubali na ukaamua kuacha huo uchangu ndo hivyo hivyo uendelee na mwendo huo huo hakuna cha kusema eti mi nimeshindwa we jijenge tukisaikologia kila kitu kitaenda sawa pia utubu sana kwa Mungu na uombe akusaidie usiwe na mawazo hayo na kweli itakuwa hivyo,jamani tujitahidi sana kuziheshimu ndoa zetu

    ReplyDelete
  3. daaah, dada hiyo ni tamaa, kweli mwenzio kakutoa kwenye ukahaba akakupa heshima akakuoa, leo unadiriki kuenda kujiuza tena, je ukimletea ukimwi ndani utaisikiae, plzz acha kua mbinafsi, kwann tunapenda kuwategemea wanaume kwa kila kitu?? kama unaona anakupa hela kidogo kwann usifikirie kuanzisha biashara unaona utaimudu?? am sure ukikaa nae chini kumwambia aidea yako ya biashara na mtaji akutafutie, cdhani kama atakataa, jishughulishe mamii, sio kwenda kujiuza, kaa chini uongee na mumeo umwambie kitu gani unataka, ndoa si rahisi dada angu. tafadhali acha kujiuza.
    fatma

    ReplyDelete
  4. Unauliza jibu???
    We mwehu kweli.
    Kama huyawezi mwambie akupe talaka

    ReplyDelete
  5. acha kujitia wazimu bure au una pepo la ngono?

    ReplyDelete