Monday, May 24, 2010

VYOO VYA NJE JAMANI......


tunajua ya kwamba wengi wetu huishi maisha yakawaida tu ya kiafrika na tunakaa kwenye nyumba zile za kawaida tu choo, bafu vyote vipo nje tofauti na watu wachache wenye uwezo wakuishi kwenye nyumba ambazo vyoo, na bafu vipo ndani na wengine wenye bahati zaidi hata vipo chumbani mwao wanapolala...

jamani vyoo na mabafu yetukwakuwa vipo njeya njumba zetu basi visitupe sababu ya kufanya mambo ya ajabu, utakuta baba anaenda chooni amevaa taulo fupi linaloonyesha miguu yake na ilivyokuwa na manywele mpaka kichefuchefu, ama utamkuta mwanamke anatoka na kanga moja anaenda bafuni ama kuswaki jamani haipendezi mnatafuta nini maneno ama kuchekwa maana vitu vyenyewe vya kuvutia hamna sasa kwanini msijistiri miili yenu?

na wengi wanakaa nyumba za kupanga mara baba haupo mkeo katoka na kanga moja labda kaka chumba cha pili kavutiwa nae basi kiulaini unasaidiwa maana wanaume kwa kuomba mpaka wanatia huruma...

na wewe baba ndio umetoka na hicho kitaulo mara kimekudondoka dada wa jirani kaona mambo ambayo hata mpenzi wake hana unadhani kitatokea ni ni dada atajilengesha mpaka uingie mkenge na hivi wengi mlivyokuwa wadhaifu??????

jamani tujitahidi kuepuka tusiyoyategemea haswa tukiwa tunawakwaza wale tunaoishi nao karibu....

0 comments:

Post a Comment