Friday, March 15, 2013

Mwanaume lako hili kama linakuhusu..

Jamani leo nataka niongee na wanaume na kama unajuwa hili linakuhusu naomba weekend hii ukirudi nyumbani ubadilike na ulitendee kazi.

Kuna wanaume wengine jamani yani kama hajakuoa ndio uboyfriend tena akikupigia simu mkakutane mfanye mambo yenu unaanza kujiuliza mara mbilimbili sijui niende au nimsingizie kitu kimenitokea au ndio ukiona unaenda kwake unaamua kabisa kuvaa pad ili usiguswe..hehe heiya

Yani mwanaume hujui starehe ya mzunguko unalazimisha kama bondea unazani upo mechini hapo unatafuta ushindi inahusu!! mwanaume utakuta mkifika kitandani mpaka anvuta pumzi yani anajiweka tayari kwa tendo na akiingia yeye vurugu anacharua uke kama anafungua kitabu anatafuta pakuingia yani hakuna maandalizi na akiingia sasa anavyofanya kwa haraka na kwa nguvu jamani kama unataka kushindana nguvu siukawatafute wakina matumla huko mkapimane ubabe..ebo

Nakwambia atakubinuabinua kama samaki anakaangwa atakupinda kama anapinda upindo kwa nguvu na haraka huku anahema kama anaendesha farasi aliyekwambia ukifanya hivyo ndio utaoneka mjuzi wa mapenzi nani ama unajuwa wataalamu wa mapenzi ni wanaofanya hivyo wanaume wengi hawajui kuzungusha ilimradi kaingia na kutoka na kukupindapinda basi yeye ndio anajiona hodari..kumbe mwanamke wako moyoni ankung'ong'a tu umalize haraka apumzike maana hizo kunja mwisho miguu inamtetemeka kama ana degedege..inahusu

Ukiulizwa kwanini humuandai mwanamke wako eti muda unaenda huku mimi nimeshasimama naumia alaa sasa mwanamke gani anayetaka mwanaume wa aina hii mwenzangu utatupwa huko kwenye dustbin  mwanaume ujuzi siku hizi bwana kitanda hakina cha mwanamke wala mwanaume siku hizi pasu kwa pasu natoa maujuzi yangu unanipa yako na kama wewe ndio wa wa haraka baba utakimbiwa, bora kama hujui mapenzi ukamuomba mwanamke wako akufundishe ndio maana sisi tunafundana mara kwa mara wanawake waelewe nini cha kufanya kwenye kitanda na kuwapa raha wapenzi wao na wao wenyewe kujipa raha.

Mwanamke anauwezo wa kumfundisha mwanaume wake mapenzi na ikawa siri ila mwanaume akikutana na mwanamke ambaye hajui mapenzi itatangazwa kila kona yule muone vile hana lolote, na raha ya mzunguko mfundishane mwambie nikifanya hivi unajisikiaje na yeye akikuambia ukifanya hivi nasikia hivi kwahiyo fanya vile tena na wewe ndio usije ukasimamamisha mshipa kama umeona nini sijui kubali mapungufu yako na yafanyie kazi..

 


0 comments:

Post a Comment