Thursday, November 8, 2012

Vituko Uswahilini....

Dada Rose

Uswahili kweli kuna vituko ila mimi nataka nikupe kisa cha mtaani kwetu kuna baba mmoja ameoa na anawatoto wa tatu wakubwa tu huyo mtoto wake wa kwanza ni mdada anafanya kazi kwenye bank moja maarufu sana hapa jijini sitamtaja jina wala bank anayofanya kazi.

Huyu mdada anatabia mbaya sana ya kufanya mapenzi na baba yake na kumbe ni kwanzia muda mrefu sema ilikuwa sirisiri lakini limegundulika nakwambia bado motomoto mtaani kwetu, mama yake alisafiri kwenda kijijini kwao kulitokea na msiba na yule baba alikataa kwenda na hakuna mtoto yoyote aliyenda na mama yake kwenye msiba cha kushangaza zaidi. 

Sasa vituko vilianza pale yule dada mkubwa ilikuwa wakishaenda kulala kila ikifika saa sita usiku anaawaambia wadogo zake kwamba anaogopa kulala peke yake anaenda kulala na baba chumbani, ukawa ndio mtindo wao kila mara siku hiyo mdogo wake mmoja akamwambia dada hata mimi leo ukienda kulala na baba na mimi pia nitakuja nataka na mimi leo nikalale chumbani kwa baba.
Yule dada akawa kama amekasirika na kumwambia mdogo wake kwaniniukalale usilale hapa, yule mdogo mtu akakubali asiende kulala chumbani kwa baba yao, kama kawaida yule dada usiku akatoka akaenda kulala chumbani wa baba yao, yule mtoto alipoona dada yake ameondoka akasubiri kidogo baada ya muda anasema aliamua kwenda chumbani kwa baba yao.

Akafungua mlango taratibu na kuchungulia ndani akamkuta baba mtu ananeng'eneka kwenye kiuno cha mwanaye akaangalia kwa muda ili ahakikishe anachokiona ni sahihi akatoka na kumueleza yule ndugu yake mwengine kwakuwa waliogopa kumshtua mama yao wakaenda kumwambia baba yao mkubwa anaishi hukuhuku buguruni mjomba akawashauri wrudi nyumbani kwamba atakuja kesho yake na wazee wenzake.

Yule mjomba bila kuchelewa akampigia shemeji yake simu ambaye ndio mama yao kwamba arudi nyumbani kuna jambo, kweli yule mama akarudi kutoka safaro mumewe anashangaa vipi mke wangu mbona unarudi bila taarifa ndio mkewe kumuhadithia kuhusu simu ya shemeji yake.

Kesho yake shemeji yake kuja na wazee wengine watatu basi wambea wa mtaa wakadhani mtu kaja kuposwa siunaelewa tena uswahilini mara wakakaa kikao ndio shemeji yake kuleleza kila kitu alichoambiwa na mdogo mtu basi wale kuulizwa hawajakataa na wakakubali kwamba ilianza muda mrefu walikuwa wanakutania gesti basi yule mama kusikia hivyo akapiga ukunga kwanguvu na  akazimia.

Majirani kusikia ule ukunga wakajuwa kuna jambo sindio kwenda vipi tena hapa maneno ya chinichini yakaanza mpaka ikajulikana tatizo watu ndio huh!! kushikwa na butwaa kuanza kumsuta yule msichana tena siunaelewa uswahilini watu wanavyojuwa kununua kesi baadaye wakamuhudumia yule mama akaamka lakini akawa hana nguvu ikabidi kikao kiahirishwe wampeleke hospitali.

Baada ya siku moja mama akatoka hospitali ndio kurudi nyumbani shoga yule mama aliongea maneno kuhusu mwananye akamwambia jinsi alivyompa tabu alivyozaliwa bado kidogo amtoe roho leo anaenda kuwa hawara wa baba yake!!!! yule mama alilia jamani basi wazee wakapanga wachinje wasuguliwe na dawa za kienjeji wanye na damu waondoe ile laana isiharibu vizazi basi ikafanywa hivyo lakini mpaka sasa yule mama kawa kama kachanganyikiwa hataki kabisa kuongea na mwanaye wanapigana tu vikumbo kama mke mwenziye, yule mtoto hata aibu hana na yeye kaganda tu pale nyumbani hana hata habari ya kuama kumaliza soo, baba mtu ndio hababaiki kama hakuna baya alilofanya.

Aibu hii jamani


0 comments:

Post a Comment