Sunday, November 11, 2012

Mmmmhhh Makubwa haya

huyo shoga anadai alimfumania Aunty Ezekiel na mumewe siku 21tu baada ya kufunga ndoa...

Tatizo siku hizi mapenzi yashakuwa poapoa tu watu wanaolewa kutoa nuksi kwao sio kwamba ni agano ambalo MUNGU ameliweka, ndio maana utakuta kwenye reception ya harusi hawara ya mumeo yupo palepale kaja kumsoma mkewe na sendoff ya mkeo hawara yake pia yupo kaja kumsoma mumewe yani siku hizi ndio maana na mambo ya ajabu hayaishi kama kugandana na watu kuuana kisa mapenzi.

Hakunaga mapenzi siku hizi..TUKO WANGAPI kwa mumeo mnaweza kuwa kumi na kwa mkeo mpo kumi mjihesabu sasa.. na kwa namna hii ukimwi utaisha kweli utakuta mtu mkewe anajitunza halafu mwanaume anamletea ukimwi ama mwanamume anajitunza mkewe anamletea mumewe ukimwi..mmhh hapana

MUNGU hapendezwi na hii tabia hapa duniani tunapita malipo huko tunapoenda tuone huo uzuri wako unaoringa nao duniani mbinguni utakufanyaje usipobadilisha maisha yako.

0 comments:

Post a Comment