Monday, August 13, 2012

kila mtu na mtu we kama wewe mwizi hii haikuhusu, tafuta wako..Tajibeba

 Macho yameona wengi lakini hayakuamua, yeye kunipenda mimi kipo kilichomvutia..kwenye mapenzi nipo juu asilimia mia kwa mia, nampeti namuenzi kila raha za dunia,  wala simnyimi kitu rukhsa nimemuachia kwa utaalamu wake tu kibali nimeshamridhia...hehe heiya

Sikuanza jua lichomokapo na giza hutanda juwa lizamapo, moyo hupoa kizuri ukipatacho, sina cha kukuombea zaidi ya maisha marefu, tunu nimetunukiwa kati yenu nyie maelfu..sema wee mama mashauzi

Siri ipo siri ipo kwa manani sio hapa duniani, siwafichi abadani siri yangu siri yangu ya moyoni..hallooooooooooo

 La kwanza ni mkarimu akiwa namimi ndani, tena hapendi kunidhulumu ananienzi kwa hisani, na pia ni msikivu akiwa nami ndani, tena anaelewa ni wapi anishike..hehe heiya Lako hilo 

Tumependana mimi na yeye acheni jealously zenu tusharidhiana wenyewe hatujawaomba chenu..

Lako hilo jito upati baridi maisha yako, miye yuleeeeeeee utaniona hivhivi la kwangu hulipati ng'o

0 comments:

Post a Comment