Tuesday, May 8, 2012

SOMO.....

Leo nataka kuongelea utumwa wa mapenzi, wewe mwanaume/mwanamke unapoamua kuingia katika uhusiano na mwenzako unategemea nini, unamweleza mwenzako kwamba nataka hivi na hivi kile sikitaki na mwenzako pia natumaini anakueleza apendayo.

Wanaume mtaniwia radhi siwasemi vibaya lakini asilia kubwa ya wanaume hugeuka na kufanya tofauti ya makubaliano wakati wanawake hukaa katika mstari, kwamba hutaki nilewe sitalewa, hutaki niwe na mwanaume mwengine fine nitakuwa na wewe lakini nyie mmmhhh mara nyingi hata moja hamfanyi.

Tuje kwenye kuchuma tunda, mwanaume anakwambia mimi napenda unifanyie hivi mpenzi basi wewe unamfanyia bila tatizo tena kwa mahaba yote sasa ikifika wewe style anayokuweka haikufikishi ama unaumia ukimwambia anasusa!!!! na hii nimesikia kuwatokea wanawake wengi tu

Kuchuma tunda ni tendo ambalo wote mnatakiwa kulifurahia, sio mmoja anafurahia na mwengine anaumia hatakama mnapendana vipi pendo la kwanza nikuweza kumfikisha mwenzako hiyo ndio sifa ya kwanza katika mapenzi halafu unaposusa unamaanisha nini?

Wanawake wengi wamekuwa watumwa kwenye mapenzi mwengine jana ananiambia amekuwa kwenye mapenzi na mwanaume mtu mzima kwa miaka mitatu anaweza kukumbuka labda ni mara tatu tu yule baba amemfikisha kileleni, siku zote anamvumilia kwasababu yule baba anamuhonga hela sana, ameshamnunulia gari, anamlipia kodi ya nyumba na kumlea mtoto wake aliyezaa huko nyuma kwahiyo she cant afford kumuacha huyu mtu kwahiyo yupo tayari kuwa na mwanaume wa pembeni wa kumfikisha kileleni lakini asimuache yule baba wakati yule baba yeye anajuwa wakati wote anamfikisha kileleni.

Mpenzi unafki ni mbaya kama mwenzako hakufikishi ama unapenda kuwekwa style tofauti mueleze mwenzio, mimi nitakwambia mpenzi hapa nope kaa hivi ukikasirika na kususa then utakuwa umeamua kufanya hivyo lakini hayo sio mapenzi ya kweli utakuwa umeamua kuwa muongo na kutomthamini mwenzako.

 A special friend of mine once told me, mwili wako ndio kitu pekee cha thamani ulichokuwa nacho.




0 comments:

Post a Comment