Wednesday, February 27, 2013

Hapo sasa..

Unapooa au kuolewa unaambiwa kuwa ukiwa na tatizo mueleze msimamizi wako wa ndoa, tumeshuhudia wengi wakilia kuwa siri zao za ndoa zimevuja sababu alimuamini msimamizi akamsimulia ili amsaidie au aombe naye na msimamizi akazisambaza kwa watu.

Je, ukipata matatizo kwenye ndoa hua unamweleza nani? Mama yako, dada, kaka, wifi, mchungaji, mama mchungaji, shemasi, shost, mzee wa kanisa au unamuomba Mungu pasipo kumwambia yoyote? Kumbuka matatizo mengine yanahitaji ushauri wa mtu mwenye hekima na busara.

Source: Women of Christ

0 comments:

Post a Comment