Tuesday, May 3, 2011

MANENO YA MAHABA KWA MPENZI WAKO....



leo nataka kuzungumzia maneno ya mahaba, jamani tunajuwa ya kwamba ukiwa na mpenzi wako unafurahi zaidi pale japo muda fulani atakupa maneno matamu, na mazuri na yenye kuzidi kukupa moyo wa wewe kuzidi kutaka kuwa naye...


sasa kuna wapenzi wengine hata mimi nilishapitia mmoja wakati fulani, jamani wanaume na wanawake wenzangu hebu tujitahidi maneno kama mpenzi, honey, sweety, mkiwa mbele za watu kumuita mpenzi wako sio mbaya maana wengine haswa waliozaa utasikia baba fulani mara mama fulani inamaana baada ya kuzaa mpenzi, sweety, honey umeisha?????? tunawapenda sana watoto wetu lakini wao wananafasi yao na mwenza wako ananafasi yake...


kwenye sita kwa sita watu utawakuta kimya tu madai wanasikilizia uhondo, jamani kuna maneno pale ama mnaoneana aibu sasa kwangu raha mpenzi aongee aniambie anavyojisikia wapi niongeze, vipi nikae, wapi nimshike kwa sauti ya taratibu na yenye mapenzi tele....sijui wewe mwenzangu


sasa pakiwa kimya tu jamani na ndio kwa mfano kitanda ndio vileeee ukigeuka tu majirani mpaka watujuwa hizo kwinyo kwinyo kwinyo hapo kwenye mechi sindio balaa maana utakuwa usikilizii raha unakilaani kitanda tu hichi nacho mpaka watu wajuwe leo napewa.....


kama mnaona aibu kuongea basi kama chumbani kuna redio wekeni hata mziki wa taratibu kuwahamasisha zaidi, maana ule ndio utakaoongea kwa niaba...


maneno ya mahaba jamani ndio mafuta tosha ya kuendesha hilo gari la mapenzi...

3 comments:

  1. Darasa zuri sana hapa. kama wengi wangelipata hakika kungekuwa na mabadiliko:-)

    ReplyDelete
    Replies
    1. mrs ngonyani iknowu somehow,but idontknow what youmean whenyousay
      goodclass. if others theywas archived sure therewas changes, how?and what youmean, teellme myname is
      TELESIO-PETER
      MY EMAIL: telesiopeter@gmail.com

      Delete
  2. naipenda sana hii blog big up!

    ReplyDelete