Tuesday, August 27, 2013

ULIMI..

ULIMI ni nyama laini sana ambayo huungua na kupoozwa kwa haraka sana, ulimi usipousafisha vizuri hufanya mdomo kutoa harufu mbaya sana, ulimi ni wa heshima na unatakiwa kutunzwa sana ndio maana ukafichwa ndani ya mdomo huonekana pale panapotakiwa tu..ulimi wapendwa ndio hubeba maisha yetu, hubeba mahusiano yetu na hubeba ndoa zetu ulimi wako unaongeaje wewe, unaiambia nini jamii, unaambia nini watoto wako, unamwambia nini mume/mke wako ndoa nyingi zimevunjika na hazina raha kwasababu ya ulimi wetu, mumeo/mkeo anapokosa unaanza kupayuka matusi na maneno ya kashfa, au tena mama mkwe na ma wifi ukiwaamlia mbona wanajuta kumjua hata huyo ndugu yao..lakini ukijuwa kutumia ulimi wako vizuri utapata baraka katika ndoa yako watu wa nje wakiiona watatamani wawe kama wewe, ndoa zilizo dumu zaidi ya miaka 20 usidhani wao yaliwanyookea tu hapana bali walijuwa kugombana na kuongea kwapamoja vizuri, ULIMI unachachua na kulainisha kwa wakati mmoja jua kuchuja maneno yako ukiwa unaongea na mumeo/mpenzi wako ili uwe na amani na upendo wa kweli utawale maisha yenu.

0 comments:

Post a Comment